Huko kwingine kwawaka, damu ingali kondeni,
Vilio vinasikika, hakukaliki jimboni,
Huzuni imetufika, kila kutwa kaburini,
Tumeni ndege mweupe, mwekundu ana majanga.
Hata muweke lawama, Mungu ndiye ataweza,
Huyo ndiye wa rehema, baya likijitokeza,
Huyatenda yalo mema, bila yeyote kubeza,
Tumeni ndege mweupe, mwekundu ana majanga.