Fikiri kuhusu mandhari yenye hewa safi. Kila mwananchi hupendezwa na eneo safi anakoishi. Lisome shairi hili lenye sifa si haba za jiji… Sifa za Jiji


Sifa za Jiji

Ninalitazama jiji, lenye wingi kupendeza,
Wahandisi kwa vipaji, matajiri kuwekeza,
Majumba yaliyopangwa, kama haya ya kuumbwa.

Usafi na usafiri, wa mfano kupigiwa,
Mandhari ya bahari, ndiyo bora kusifiwa,
Mpangilio dhabiti, jiji linalopendeza.

Nchi kavu na angani, wasafiri waridhika,
Kandawala yu makini, waendako wakafika,
Hili jiji lina mema, wakazi wafurahia.

Milimani kuna watu, mabondeni hawakosi,
Uzuri wao ni utu pasipo na la uasi,
Ni jiji lililo jema, wema usio kifani.

Wema wa hali ya hewa, tena inayovutia,
Si jua na si mvuwa, hewa ya kufurahia,
Jiji linalopendeza, linalo wingi wa sifa.

Hamna la ukabila, uraia ndio hoja,
Yapo muhimu maswala, ya kunufaisha waja,
Mji bora kwa watu, uishi na kuwekeza.

Utawala ndio mwema, jiji hili kushamiri,
Duniani unavuma, kwa zake njema habari,
Jiji linajulikana, kwa sifa kadha wa kadha

Maoni 1 kwa “Sifa za Jiji”

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *

*