Kuhusu Kĩmani wa Mbogo

Kimani wa Mbogo ni mwandishi na mtunzi wa mashairi nchini Kenya.

Penzi Langu la Moyoni

Shairi hili linazungumzia hisia za dhati za upendo na jinsi mhusika mkuu anavyomthamini mpendwa wake. Amejieleza kwa kina na hisia kuhusu umuhimu wa mpenzi wake maishani mwake, akilinganisha penzi lake na mambo mbalimbali yenye thamani kubwa. Mpendwa wake anaonekana kama dawa ya majonzi, msuluhishaji wa shida, na kama malaika wa moyoni mwake. Shairi hili linasisitiza uzito wa upendo na jinsi unavyoweza kubadilisha maisha ya mtu, na linatufundisha thamani ya kuthamini wale tunaowapenda. Shairi hili ni tafsiri ya kina ya hisia za upendo zisizo na kipimo. Penzi Langu la Moyoni

Jibwa Litaniumia Toto

Sijui kama unamfahamu vema jirani yako au mtu mnayeshirikiana naye kwa karibu mno. Na suala la “Nyumba Kumi”  linapotajwa sijui linaibua hisia gani kwenye fikra zako. Baadhi ya watu tunaoishi pamoja, huenda wasikufae kwa chochote au lolote.

Wengine watakutumia, wakunongeshe na kukudhalilisha, hasara kwako. Wengine ni wanafiki wasio na utu, wasiokutendea lolote la hisani. Hata kama utamwamini aliye karibu nawe, usimtegemee wala ukadhani ni malaika kwako. Hili halimaanishi wewe usimtendee wema. Tenda wema nenda zako.

Shairi lifuatalo linaelezea kwa kina suala hili. Mhusika anahofia kwamba mtoto wake ataumwa na jibwa la jirani. Hili lalinganishwa na maovu anayoweza kufanyiwa na jirani yake. Ni shairi linaloonya kuhusu ushirikiano wako na jirani au mwandani wako wa karibu. Linamfahamisha hatari zinazomkabili kuwa na jirani asiye na matendo mema. Jibwa Litaniumia Toto