Kutwa ninahangaika, niko nalo hangaiko,
Inanibidi kumaka, nikakumbwa na kimako,
Nipate wapi karadha, mkopo usio riba?
Nendapo ili nikope, ni bure kwamba sikopi,
Naharibu niihepe, Kumbe riba siigepi,
Nipate wapi karadha, mkopo usio riba?
Riba imekuwa hewa, unapotaka mkopo,
Tena wameiinuwa, iso riba isiwepo,
Nipate wapi karadha, mkopo usio riba?