Kijacho Kinapokuja
Wapo baadhi ya watu wasiopendezwa na utu. Hutenda kinyume cha matakwa ya binadamu. Anapotenda, jamii humgeuka na kumtendea, kijasho kikamtoka. Litazame shairi hili… Kijacho Kinapokuja
Kitovu cha Ushairi, Washairi na Mashairi
Wapo baadhi ya watu wasiopendezwa na utu. Hutenda kinyume cha matakwa ya binadamu. Anapotenda, jamii humgeuka na kumtendea, kijasho kikamtoka. Litazame shairi hili… Kijacho Kinapokuja
Usijifanye kasuku kuiga kila jambo. Yawache ya wengine. “Unavyopenda kuiga, kutwa moja utajuta” Kutwa Moja Utajuta
Sijui kama unamfahamu vema jirani yako au mtu mnayeshirikiana naye kwa karibu mno. Na suala la “Nyumba Kumi” linapotajwa sijui linaibua hisia gani kwenye fikra zako. Baadhi ya watu tunaoishi pamoja, huenda wasikufae kwa chochote au lolote.
Wengine watakutumia, wakunongeshe na kukudhalilisha, hasara kwako. Wengine ni wanafiki wasio na utu, wasiokutendea lolote la hisani. Hata kama utamwamini aliye karibu nawe, usimtegemee wala ukadhani ni malaika kwako. Hili halimaanishi wewe usimtendee wema. Tenda wema nenda zako.
Shairi lifuatalo linaelezea kwa kina suala hili. Mhusika anahofia kwamba mtoto wake ataumwa na jibwa la jirani. Hili lalinganishwa na maovu anayoweza kufanyiwa na jirani yake. Ni shairi linaloonya kuhusu ushirikiano wako na jirani au mwandani wako wa karibu. Linamfahamisha hatari zinazomkabili kuwa na jirani asiye na matendo mema. Jibwa Litaniumia Toto
Werevu huwa na wingi wa busara. Ni muhali kuwapata wakifarakana au wakigombana. Tofauti zao husuluhishwa bila ghasia. Hukosi wengine wasiolielewa hili. Wapo wasioithamini heshima wala busara. Hufarakana pasi na sababu. Lisome shairi hili uelewe ukweli huu. Werevu Huelewana
Wanaopayuka huudhi mno. Watasema chochote bila kujali wala kuchunguza. Huwa ndio asili ya lolote linalosemwa bila kujali. “Kidomodomo waudhi, kupayuka kwanongesha!” Kupayuka Kwanongesha