Penzi Langu la Moyoni

Shairi hili linazungumzia hisia za dhati za upendo na jinsi mhusika mkuu anavyomthamini mpendwa wake. Amejieleza kwa kina na hisia kuhusu umuhimu wa mpenzi wake maishani mwake, akilinganisha penzi lake na mambo mbalimbali yenye thamani kubwa. Mpendwa wake anaonekana kama dawa ya majonzi, msuluhishaji wa shida, na kama malaika wa moyoni mwake. Shairi hili linasisitiza uzito wa upendo na jinsi unavyoweza kubadilisha maisha ya mtu, na linatufundisha thamani ya kuthamini wale tunaowapenda. Shairi hili ni tafsiri ya kina ya hisia za upendo zisizo na kipimo. Penzi Langu la Moyoni

Kwangu Huwa Maridhia

Mapenzi ni jambo la mtu na hiari yake. Hulazimishwi kumpenda huyu ama yule. Wengine watakuvunja moyo na kukwambia unayempenda si mwema. Kila mtu ana ila zake. Hakuna mwanadamu aliye kamili asilimia mia moja. Unapozitambua ila za mke wangu, jua na usinipashe kwa kuwa nilizijua kitambo. Wengine watakupasha mengi yasiyo na maana wala ukweli kuhusu mpenzi wako ili umwache amtongoze. Mara nyingi udaku hupotosha na kuangamiza wawili wapendanao ama hata familia.

Shairi lifuatalo la tarbia lina mengi ya kufahamisha. “Sijali mnavyomwita, kwangu huwa maridhia”. Hata mseme, mmbadike majina ama mmdharau, kwangu nampenda tu. Mpenzi wa mtu ni mpenzi wake tu yawache ya kwao huyawezi. Hebu lisome na utafari kwa kina. Ufurahiae uhondo wa shairi hili la Kimani wa Mbogo analoliita “Kwangu huwa maridhia”. Kwangu Huwa Maridhia