Umuhimu wa Mashairi

Mashairi yana umuhimu wa kipekee katika jamii kama ifuatavyo:

  • Kuibua hisia za kuburudisha na kuhuzunisha
  • Kukosoa, kukashifu na kubadilisha tabia zisizofaa katika jamii
  • Kupasha ujumbe  kwa hadhira kwa njia ya mvuto
  • Kuelimisha, kuhamasisha na kuzindua jamii
  • Kuhifadhi matukio muhimu ya historia ya jamii
  • Kuhifadhi na Kuendeleza Utamaduni
  • Kukuza Ushujaa, Ujasiri na Uzalendo
  • Kufikirisha na kunoa fikra
  • Kuliwaza
  • Kuonya, kutahadharisha, kunasihi na kuelekeza
  • Kuadilisha na Kuadibisha
  • Kusifia mtu au kitu
  • Kuendeleza na kukuza kipawa cha utunzi
  • Kupamba, kukuza na kuineza lugha
  • Kuhifadhi msamiati wa lugha ya Kiswahili na Sanaa ya fasihi
  • Kuburudisha hadhira na wasomaji
  • Kukejeli au kukemea mambo yanayoenda kinyume na maadili ya jamii
  • Kuwasilisha hisia za ndani za mtu na mawazo