Mizani ni ulinganifu wa idadi ya silabi katika kila kipande au mshororo wa ubeti wa shairi.
Tazama mshororo huu:
“Mola ndiye hutulinda, inapokuwa tuhuma.”
Tunagawanya mshororo huwa kwa vipande, utafahamu kuwa mshororo huu una mizani 16. Upande wa kwanza 8 na upande wa pili 8.
Tazama hapa:
Mo-la ndi-ye hu-tu-li-nda, i-na-po-ku-wa tu-hu-ma