Siku ya kiama ikifika, kunao watalia. Wapo baadhi ambao wakuwa na furaha pia. Je, wewe utakuwa upande gani? Angani Ange Kuenga


Angani Ange Kuenga

Ja yangeyange taanga, wengi kwa wenga tawinga,
Toka kwa wingu tawanga, wengi kwa wingi taunga,
Wa kongamano takonga, si kunga wake kuunga,
Angani ange kuenga, ingawa kuengaenga.

Wa bengi bonge tatenga, tange la tonga tatenga,
Chengechenge walochenga, ndo iwe chenge tatenga,
Chango iwe tongo tenga, wanguwangu akianga,
Angani ange kuenga, ingawa kuengaenga.

Wengi watalengalenga, watazongwa na kulonga,
Kwa aloanga talenga, wa yengeyenge talinga,
Atatanga wa upanga, tarenga renge kiranga,
Angani ange kuenga, ingawa kuengaenga.

Pingwa hongo hangahanga, hangaiko ja wajinga,
Tatangatanga ja bunga, kuona aliyeanga,
Kwa nunge tasongasonga, kuungua ungaunga,
Angani ange kuenga, ingawa kuengaenga.

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *

*